UMEBEBA TEMBO, SIO MBWA: ACHA KUJILINGANISHA NA WATU

 

*Tembo na mbwa walishika mimba siku moja.*  

*Miezi 3 baadaye, mbwa akazaa watoto 6.*  

*Miezi michache ikapita, mbwa akazaa tena wengine 8.*  

*Akazaa tena. Na tena.*  

*Ndani ya mwaka mmoja akawa na kizazi kikubwa. Watoto wake wakaanza kuzaliana hapo hapo.*  


*Siku moja mbwa akamsogelea tembo na kumuuliza kwa dharau:*  

_"Ndugu, una uhakika una mimba kweli? Tulishika siku moja. Mimi nimeshazaa mara 4. Nina watoto zaidi ya 20. Wewe hujazaa hata mmoja. Kuna shida gani?"_


*Tembo akatabasamu. Akamjibu kwa utulivu:*  

_"Ndugu yangu, sikiliza. Mimi tumboni sijaubeba mbwa. Nimeubeba tembo."_  

_"Nitamzaa baada ya miaka 2. Lakini akizaliwa, akigusa ardhi, dunia nzima itatetemeka."_  

_"Watoto wako wanapoishiwa na chakula, wanakula takataka."_  

_"Mwanangu akitoka, akitaka kuvuka barabara, magari yatasimama. Watu watashangilia. Watapiga picha."_  

_"Watoto wako 100 hawana thamani ya mtoto wangu 1."_  


*FUNZO KWA MWANAUME ANAYEJILINGANISHA:*  


*1. ACHA KUHESABU WATOTO WA MWENZAKO.*  

Mbwa anazaa haraka. Watoto wake ni wengi, lakini ni wa kawaida. Tembo anazaa mmoja baada ya miaka 2, lakini anazaa MTAWALA.  

*Rafiki yako amenunua boda boda. Wewe bado unasave ya gari. Usilie. Unabeba gari, sio boda.*


*2. KILA KITU KIKUBWA KINACUKUA MUDA.*  

Nyumba ya udongo inajengwa siku 3. Ghorofa inajengwa miaka 3.  

*Kama maisha yako yanachelewa kufunguka, maana yake unajenga kitu kikubwa. SAJAS anataka matokeo ya kesho. MWANAUME anasubiri matokeo ya miaka 5.*


*3. THAMANI HAIPO KWENYE WINGI. IPO KWENYE UPEKEE.*  

Mbwa 100 hawafiki thamani ya tembo 1.  

*Biashara zako 5 za TZS 100K hazifikii biashara 1 ya TZS 10M.*  

*Acha kukimbiza vitu vidogo vidogo. Jikite kwenye kitu kimoja kikubwa.*  


*HIVYO SAFARI YAKO, ACHA KUILINGANISHA NA YA MTU MWINGINE.*  

*Hakikisha ulichokibeba wewe dunia ikikiona itajua ni tofauti.*  

*Wewe si mbwa. Umebeba tembo.*  


*Swali kwako:*  

*Je, wewe unajua unabeba nini tumboni mwako? Au unazaa tu mbwa kwa sababu unaona wenzako wanazaa?*  

*Comment chini. Tupe ushuhuda.*


*#UkweliMchungu #TemboNaMbwa #Subira #Mafanikio

Comments

Popular posts from this blog

CHUKUA ELFU 50,000: SIRI YA KUTOFANIKISHA MAISHA YAKO

ULIISHA ACHWA KISA HUNA PESA? HII NDIO SABABU MWANAUME TAJIRI HAACHIKI.

SPY NA BOSS WA MILLION 5: SOMO LA KIKATILI KUHUSU KUJIAMINI, KAZI NA THAMANI YAKO